Kikao cha maandalizi ya mkutano mkuu wa 18 wa Chama cha Kikomunisti cha China kimefanyika leo alasiri hapa Beijing chini ya uenyekiti wa rais Hu Jintao.
Kikao hicho kimepitisha orodha ya wajumbe 22 wa tume ya uhitibishaji wa wajumbe wa mkutano mkuu wa 18 wa Chama cha Kikomunisti cha China, na orodha ya wajumbe 247 wa kamati ya utendaji ya mkutano huo. Kikao hicho kimemteua Xi Jinping kuwa katibu mkuu wa mkutano huo.
Kikao hicho pia kimepitisha ajenda wa mkutano mkuu wa 18 wa Chama cha Kikomunisti cha China, na kutangaza kuwa, mkutano huo utafanyika kuanzia tarehe 8 hadi tarehe 14 mwezi huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |