Kikao cha kwanza cha kamati ya utendaji ya mkutano mkuu wa 18 wa Chama cha Kikomunisti cha China kimefanyika leo alasiri hapa Beijing.
Rais Hu jintao wa China amehudhuria kikao hicho na kutoa hotuba muhimu.
Kikao hicho kimepitisha orodha ya wajumbe 41 wa Halmashauri ya kudumu ya Kamati ya utendaji ya mkutano mkuu wa 18 wa Chama cha Kikomunisti cha China. Pia kikao hicho kimepitisha ripoti ya tume ya uthibitishaji wa wajumbe wa mkutano huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |