Viongozi, vyama na mashirika ya nchi mbalimbali duniani yameupongeza Mkutano mkuu wa 18 wa Chama cha Kikomunisti cha China unaoendelea hapa Beijing.
Katibu mkuu wa Chama cha wafanyakazi nchini Jamhuri ya Congo amekisifu Chama cha Kikomunisti cha China kwa kufanya juhudi za kuboresha maisha ya wananchi wa China. Amesema China imekuwa nguvu muhimu katika jukwaa la siasa la kimataifa, na mafanikio ya China yanafuatiliwa sana na dunia nzima.
Chama cha Harakati za Ukombozi wa umma cha Angola kimetoa salamu za pongezi na kusema Chama cha Kikomunisti cha China kimeijenga China kuwa nchi inayoheshimiwa duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |