Baraza jipya la serikali ya China lililoteuliwa na waziri mkuu mpya wa China Li Keqiang limepitishwa na bunge la umma la China.
Uteuzi huo umepitishwa kwenye kikao cha sita cha wajumbe wote wa mkutano wa kwanza wa bunge la umma la awamu ya 12 la China.
Walioteuliwa ni pamoja na manaibu mawaziri wakuu wanne, wajumbe watano wa taifa, katibu mkuu wa baraza la serikali, mawaziri 22, mkurugenzi wa kamati ya taifa ya afya na mpango wa uzazi, mkuu wa benki kuu ya China na mkurugenzi wa idara ya uhasibu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |