Kutokana na mwaliko wa rais Vladimir Putin wa Russia, Rais Xi Jinping wa China leo asubuhi ameondoka Beijing kwenda Sochi, Russia kuhudhuria ufunguzi wa michezo ya 22 ya Olimpiki ya majira ya baridi. Hii ni mara ya kwanza kwa rais wa China kuhudhuria kwenye michezo mikubwa inayofanyika nje ya nchi. Rais Xi pia atakutana na ujumbe wa michezo ya Olimpiki wa China wenye wanamichezo 139. Wanamichezo hao watashiriki kwenye michezo minne mikubwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |