Mgomo mkubwa wa wachimba madini ya Platinum nchini Afrika kusini umeingia katika wiki ya tano, na mpaka sasa bado hakuna dalili yoyote ya kumalizika kwa mgogo huo. Mgomo huo unaoshirikisha wachimbaji elfu 80 wa chama cha wachimba madini na wajenzi AMCU umesimamisha kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa Platinum duniani. Habari zinasema, chama cha AMCU kimeapa kuendelea na mgomo huo hadi matakwa yake yatakapotimizwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |