Naibu mkuu wa chuo kikuu cha Nankai cha China Bw. Tong Jiadong jana alisema kuwa China ilichangia zaidi ya asilimia 30 ya ongezeko la biashara duniani mwaka jana, kauli ambayo inafuatia taarifa inayotangaza kuwa China imechukua nafasi ya kwanza kwa thamani ya biashara duniani badala ya Marekani katika mwaka 2013. Bw. Tong alisema, ongezeko la biashara ya kimataifa ya China imehimiza maendeleo ya kiuchumi ya nchi na kanda nyingine duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |