Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo OECD limesema, pato la jumla la GDP la kundi la G20 liliongezeka kwa asilimia 2.8 mwaka 2013, ikiwa ni chini ikilinganishwa na asilimia 2.9 ya mwaka 2012. Katika robo ya nne ya mwaka 2013, pato la G20 liliongezeka kwa asilimia 0.8, ikiwa ni chini ikilinganishwa na asilimia 0.9 ya robo ya awali. Katika kundi hilo, China ilipata ongezeko kubwa zaidi la asilimia 1.8 ikilinganishwa na asilimia 2.2 ya robo ya awali, ikifuatiwa na Indonesia ambayo ilipata ongezeko la asilimia 1.4 sawa na ukuaji wa robo ya awali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |