Waziri mkuu wa China Li Keqiang amewasili mjini Luanda na kuanza ziara yake nchini Angola. Bw. Li Keqiang amesema, Angola ni nchi inayoibuka kwa kasi barani Afrika, na pia ni mwenzi mkubwa wa ushirikiano wa China kusini magharibi mwa Afrika. Ameeleza matarajio yake ya kubadilishana maoni kwa kina na viongozi wa Angola kuhusu masuala yanayohusu pande hizo mbili, kupanua sekta za ushirikiano kati yao katika msingi wa ushirikiano uliopo sasa, na kutia nguvu ya uhai kwa ajili ya maendeleo ya uhusiano kati ya China na Angola.