Wizara mbalimbali nchini China zimeshirikiana katika mapambano dhidi ya vitendo vya kueneza uvumi kupitia mitandao ya Internet.
Wizara hizo ni pamoja na wizara ya viwanda na habari, wizara ya usalama wa umma na ofisi ya kitaifa ya habari ya Internet. Ofisi na wizara hizo zimefunga na kuagiza tovuti kadhaa zijirekebishe ili kuimarisha usimamizi wa tovuti hizo, na kuwakamata watu walioeneza taarifa za uvumi kwenye tovuti za Internet.
Wizara hizo zimesisitiza kuwa, vitendo vya kueneza uvumi kwa kutumia mitandao ya intenet vinavunja sheria na kuharibu maslahi ya taifa na raia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |