• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Manchester United yawapiga marufuku mashabiki wake kuingia uwanjani na Ipad

    (GMT+08:00) 2014-08-13 15:31:46

    Manchester United imewaonya mashabiki wake wote kwamba hawataweza kuingia na Ipad au simu zozote za tablet ndani ya uwanja wa Old Trafford katika msimu huu. Kumekuwa na tabia ya mashabiki kurikodi mechi kupitia simu za Apple na klabu inawasiwasi kuhusu kutofuta sheria za hakimiliki. United sasa imewaonya mashabiki kuhusu sera zao mpya kupitia barua pepe, kufuatia mechi ya kirafiki iliyochezwa jana usiku dhidi ya Valencia. Barua pepe hiyo imeandikwa " tunataka kuwafahamisha kuhusu sera mpya za klabu kuhusiana na mechi za nyumbani. Mashabiki hawaruhusiwi kuingia na vifaa vikubwa vya elektroniki vyenye ukubwa wa mm150 kwa 100 ndani ya uwanja."

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako