Michezo ya Olimpiki ya Vijana inaendelea mjini Nanjing, China. Katika mashindano ya mbio ya mita 1500 kwa wanaume yaliyofanyika jana, mwanariadha kutoka Kenya Gilbert Kwemoi alishika nafasi ya kwanza kwa kutumia muda wa 3:41:99 na kukipatia kikosi cha Kenya medali ya kwanza ya dhahabu katika michezo hiyo ya Olimpiki ya vijana. Katika mashindano ya mbio ya mita elfu tatu yaliyofanyika baadaye, mwanariadha mwengine wa Kenya Koech Moses alipata medali ya shaba. Moses alisema anaridhika na matokeo hayo na kutarajia kupata maendeleo zaidi katika siku za baadaye.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |