Timu ya Uganda imeondoka juzi nchini kwake kuja China kushiriki kwenye michuano ya 6 ya mabingwa wa kombe la dunia la Woodball, ambayo yanaanza leo na kugungwa tarehe 11 huko katika kituo cha Luneng Sanya, mjini Sanya China.waziri wa taifa wa michezo Charles Bakkabulindi, ameiambia timu hiyo wakati wa sherehe za kuiaga kwamba, wachezaji lazima wawe na nidhamu mchezoni wanapokuwa China, na pia kuwatakia mafanikio makubwa kwenye michezo hiyo. Bara la Afrika litawakilishwa na Uganda, Tanzania, Kenya na Malawi. Zaidi ya timu 20 wakiwemo wenyeji China wamethibitisha kushiriki michuano hii.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |