Tyson Fury ameruhusiwa kuendelea na mechi yake dhidi ya Dereck Chisora itakayopigwa mwezi Novemba, baada ya kunusurika na marufuku kutoka kwa Bodi ya Masumbwi ya Uingereza ya Udhibiti. Hata hivyo bodi hiyo imeamua kumtoza faini Fury ya pauni elfu 15, baada ya kushtakiwa kwa utomvu wa nidhamu kufuatia kutoa maneno machafu kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika mwezi Juni. Mabondia hao wa uzito wa juu wa Uingereza watakutana tena uso kwa uso kwenye mkutano na waandishi wa habari siku ya Jumatatu. Bingwa wa Ulaya Chisora alishindwa kwa pointi na Fury walipopambana mwaka 2011. Wawili hao walikuwa wavaane tena huko Manchester mwezi Julai lakini pambano liliahirishwa baada ya Chisora kuumia mkono mazoezini.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |