Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limelaani vikali shambulizi la kigaidi dhidi ya kituo cha ukaguzi cha kijechi katika Peninsula ya Sinai nchini Misri. Baraza hilo pia limesema vitendo vyovyote vya kigaidi ni uhalifu na kamwe havitakubalika duniani. Habari zinasema shambulizi hilo limesababisha vifo vya wanajeshi 30 na wengine 28 kujeruhiwa. Wakati huohuo rais Abdel Fattah al-Sisi ametangaza miezi mitatu ya hali ya hatari katika Peninsula ya Sinai pamoja na siku tatu za maombolezi kufuatia mauaji ya wanajeshi hao wa Misri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |