• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • UNICEF kuongeza idadi ya wafanyakazi wake Afrika magharibi kupambana na Ebola

    (GMT+08:00) 2014-11-04 16:46:29

    Mratibu wa kimataifa wa Ebola kupitia Mfuko wa kuhudumia watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) Peter Salama amesema, shirika hilo litaongeza maradufu wafanyakazi wake katika nchi za Guinea, Liberia, na Sierra Leone ambazo zimeathiriwa zaidi na Ebola. Amesema watoto wanachukua asilimia 20 ya watu wenye maambukizi ya Ebola katika nchi hizo, na kwamba karibu watoto milioni 5 wameathirika na ugonjwa huo, huku watoto wengine 4,000 wakiachwa yatima.

    Amesema ugonjwa huo umesababisha kufungwa kwa shule, watoto kufungiwa majumbani na kutoruhusiwa kucheza na watoto wengine kutokana na hofu ya maambukizi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako