• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Nani asema hafikirii kabisa kurudi Manchester United

    (GMT+08:00) 2014-11-05 15:29:27

    Winga Nani amesema hafikirii kabisa kurudi Manchester United. Mchezaji huyo alikwenda Sporting Lisbon kwa mkopo na kamwe haoni dalili ya kurudi kwenye kikosi chake. Ni wazi kuwa kocha mpya wa Man United Louis van Gaal wala hamfuatilii sana hivyo Nani mwenye miaka 27 ameibuka na kusema hana mpango na klabu hiyo. Gazeti moja la Ureno la O Jogo lilimkariri akitamka: kuwa wala hana mpango wa kurudi kwenye kikosi cha Man United, kwani anawapenda watu wanaompenda, na anaamini watu wanaomuamini kuwa ana uwezo wa kufanya vizuri. Amesisitiza kuwa akiwa huko Sporting Lisbon kila anapoamka anajiona mwenye nguvu zaidi, pia kuna viongozi wanaofahamu kuwa ana uwezo mkubwa na wanataka aonyeshe kiwango zaidi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako