Shirika la ndege la RwandAir limesema kuwa linapanga kuanzisha safari katika mataifa ya Nigeria, Zambia na Ivory Coast.
Afisa mkuu wa safari katika shirika hilo Bi. Alice Katiti, amesema kwamba safari hizo zinapangwa kuanza katika muda wa miezi mitano ijayo.
Alice anasema shirika hilo ndili lililo na ndege mpya zaidi barani Afrika, na hivi karibuni watakuwa wakinunua ndege mbili aina ya Dreamliner, kutumika katika soko lao la Asia na Ulaya.
Kufikia sasa shirika hilo ufanya safari katika maeneo 17 Duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |