• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Sehemu ya Kwanza: Merikebu zenye matanga kusafiri baharini

    —Merikebu na Watu kwenye Njia ya Usafiri baharini

    Makasia sita na mashua moja ya kauri nyeusi vilivyofukuliwa kwenye sehemu ya mabaki ya utamaduni ya Gati la Hemudu la Yuyao mkoani Zhejiang China zimethibitisha kuwa shughuli za wachina kwenye bahari zilianzia zaidi ya miaka 7,000 iliyopita. Na uvumbuzi wa dira pia uliweka msingi imara kwa ajili ya kuhakikisha maendeleo zaidi ya shughuli za wachina baharini katika zama za kale. Kwa kufuata ufundi wa kuundwa kwa merikebu na mbinu za kusafiri baharini zilivyoendelezwa siku hadi siku,wachina wakaweza kufanya mawasiliano na watu wa nchi zenye tamaduni tofauti kupitia njia ya mawasiliano baharini.

    (1) Merikebu za Usafiri baharini za zama za kale

    Merikebu za usafiri baharini zikiwa vyombo pekee vya kueneza

    utamaduni wa kihali na kimali kwenye Njia ya Hariri baharini, si kama tu zilieneza utamaduni wa China hadi eneo la mbali la magharibi ya Bahari ya Uarabu, bali pia ziliwawezesha wachina wa zama za kale waelewe hali ya dunia ya nje kwa njia ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja. Ufundi wa kuunda merikebu na vyombo vya usafiri baharini vilivyorithiwa kizazi hadi kizazi vilionesha moyo wa kufanya utafiti bila kuogopa taabu waliokuwa nao wachina wa zama za kale, pamoja na kiu yao ya kufanya mawasiliano na maingiliano na dunia ya nje .


    [Mfano wa mwundo wa ndani wa Merikebu za Song ya Quanzhou]

    [Mfano wa dira ] (dira ya kuning'inia )

    [Mfano wa mashine ya upimaji wa pembe kati ya vitu viwili (ya zama hizi)]
    More>>

    (2) Wasafiri waliotaka kutimiza ndoto

    Kumbukumbu zilizowekwa kwenye historia ya China zinasema, China ilikuwa inakijua Kisiwa cha Zanzibar kabla ya kipindi cha Enzi ya Song ya kusini (kabla ya karne ya 12). Kitabu cha《Visiwa vya ng'ambo》kilichoandikwa na mtaalamu wa usafiri wa baharini Wang Dayuan wa Enzi ya Yuan(mwaka 1271-1368) kilieleza bayana, wachina wa zama za kale walifika katika Kisiwa cha Zanzibar,Tanzania zaidi ya miaka 700 iliyopita, ambapo walianza kufanya mawasiliano na waafrika.


    [Ramani ya safari ya Zheng He baharini]

    [Mfano wa kundi la merikebu la Zheng He]

    [Mtungi wenye mkono mmoja uliopakwa rangi ya kahawia]
    More>>

    Sehemu ya Pili: Maua mia yachanua

    --Kupatana na kuingiliana kwa tamaduni za aina mbalimbali

    Njia ya Hariri kwenye bahari iliyosifiwa pia kuwa ni "Njia ya biashara ya vyombo vya kauri baharini", na "Njia ya biashara ya viungo vyenye harufu nzuri baharini", ilikuwa njia kubwa ya biashara ya kimataifa katika zama za kale. Kuanzia Enzi za Qin na Han (mwaka 221 kabla ya Kristo--mwaka 220), wachina walisafirisha Hariri na bidhaa nyingine hadi India kupitia njia hiyo. Katika zaidi ya miaka 2,000 iliyopita, si kama tu bidhaa za viungo vinavyonukia vizuri, pembe za ndovu na vito zilizozalishwa sehemu mbalimbali duniani zilisafirishwa hadi nchini China kupitia njia hiyo baharini, bali pia bidhaa za Hariri, Vyombo vya Kauri na Chai za China zilisafirishwa na kuuzwa India na Afrika.

    (1) Njia ya Biashara ya Vyombo vya Kauri

    Katika karne ya 13, shughuli za utengenezaji wa vyombo vya kauri zilididimia siku hadi siku katika sehemu ya mashariki ya kati, hivyo wafanyabiashara waliojishughulisha na biashara kwenye njia ya baharini walianza kufuatilia vyombo vya kauri vya China. Ingawa kulikuwa na vyombo vya kauri vya rangi ya kijani vya Enzi ya Song ya China(mwaka 960--1279)vilivyofukuliwa katika sehemu mbalimbali barani Afrika, lakini ilipofika katikati ya Karne ya 14, ndipo vyombo vya kauri vya China vilipoanza kusafirishwa hadi pwani ya Afrika mashariki. 

    Hivi leo katika Jumba la makumbusho la taifa la Tanzania kuna vyombo vya kauri vya China vipatavyo zaidi ya mia moja vilivyofukuliwa huko, mbali na mabaki machache ya Enzi ya Yuan(mwaka1271--1368), vingi ni vyombo vya kauri vyenye thamani vya Enzi za Ming na Qing za China(mwaka1368--1912)  vilivyosafirishwa na kuuzwa ng'ambo, vyombo hivyo vinaweza kuthibitishana na vile vilivyofukuliwa kwa wakati mmoja nchini China.


    [Mtungi wa kauri wenye masikio mawili]

    [Jagi la kauri la rangi ya kijani na nyeupe lililochongwa maua]

    [Sahani yenye mapambo ya maua iliyochomwa kwenye Tanuri la Longquan]
    More>>

    (2) Njia ya biashara ya viungo vyenye harufu nzuri


    [Vipande vya magome ya mti yanayonukia vizuri (vilivyotengenezwa kwa kuiga vile vilivyofukuliwa)]

    [Fedha za kombe]

    [Vipande vya mbao (vilivyotengenezwa kama vile vilivyofukuliwa)]
    More>>

    (3)"Mji wa Mwanga" wa Quanzhou

    Biashara za bidhaa nyingi zilizofanyika kupitia njia ya baharini zilisababisha mawasiliano na hali ya kupatana katika mambo ya utamaduni kwa karne kadhaa. Mji wa Quanzhou wa China uliokuwa sehemu ya mwanzo ya Njia ya Hariri kwenye bahari, ulisifiwa kuwa ni "Mji wa mwanga", na ulikuwa mji mkubwa wa kimataifa katika karne za 12 na 13. Watu waliotoka sehemu mbalimbali duniani waliacha nyayo zao huko, na kutokana na mabaki ya kale ya utamaduni mjini humo, tunaweza kuona dalili nyingi za hali ya kupatana na kukua kwa pamoja kwa dini tofauti mbalimbali, na tamaduni za aina mbalimbali.


    [Jiwe la kaburi la "Naina Muhammad"] (lililotengenezwa kwa ustadi)

    [Jiwe la kaburi la matumbawe lenye maandishi ya Kiarabu ]

    [Jiwe lenye maandishi ya Kiarabu ya dini ya Kiislamu]
    More>>

    Sehemu ya tatu: Kupokezana kizazi baada ya kizazi

    --Uitikiaji wa zama za kusafiri kwenye njia ya baharini

    Binadamu wa hivi leo wametumia sayansi na teknolojia za kisasa kudhibiti eneo ardhini na nafasi za angani zilizo kubwa zaidi kuliko hapo awali. Lakini hulka na dhamira za kutafuta ujuzi zaidi walionao binadamu bado zinarithishwa kizazi hadi kizazi, hadithi za ajabu kwenye njia ya kale ya usafiri baharini zinawatia moyo vijana wafunge safari mpya baharini bila kusita. Mshairi kijana He Xun ambaye pia ni msanii wa China aliyezaliwa mwaka 1984, siku zote anatumia kalamu kuchora picha ili kuonesha mawazo yake juu ya historia, muda na wakati, eneo lenye miujiza pamoja na dunia ya ajabu. Na amenyanyua mwenge wa mababu zetu akitarajia kusafiri kwa uhuru akiwa na taswira nyingi akilini kama walivyo watangulizi wengi wasiohesabika ambao waliwahi kusafiri kwenye bahari ya mballi.


    [Picha za Nyota mbinguni na Myenge] (2)

    [Picha za Nyota mbinguni na Myenge]

    [Jua lachomoza mara 44 na Urukaji wa mara moja]
    More>>
    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako