Simba iliendelea kuonyesha ubabe wake katika mechi ya Nani Mtani Jembe baada ya kuichapa Yanga mabao 2-0 jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mbali na nyota wengi wa kigeni kutawala hisia za mashabiki kabla ya mechi hiyo, wachezaji wa Kitanzania, Awadh Juma na Elius Maguli waliibuka mashujaa baada ya kufunga mabao mawili ya Simba. Mabao hayo yalipachikwa wavuni katika dakika za 30 na 39. Mwaka jana Simba ilichukua ubingwa wa kombe hilo kwa kuifunga Yanga 3-1.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |