• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Klabu ya Yanga ya Tanzania yaaswa kutokuwa na uchoyo baina yao

    (GMT+08:00) 2015-01-15 14:07:19
    Kocha wa klabu ya Yanga ya Tanzania, Hans van der Pluijm amewajia juu washambuliaji wa timu hiyo kutokana na kukosa magoli mengi na kuwataka kuacha uchoyo baina yao kwa manufaa ya timu. Licha ya kushinda kwa idadi kubwa ya mabao 4-0 katika mechi zao mbili za kwanza za Kombe la Mapinduzi, wachezaji wa Yanga walikuwa wakikosa magoli mengi ambayo yangeweza kuwafanya kupata ushindi mnono zaidi. Yanga ilitolewa katika robo fainali ya mashindano hayo maalum ya kuadhimisha Mapinduzi ya Zanzibar kwa goli 1-0 la dakika za lala salama na JKU ya Zanzibar huku miamba hao wa soka wa Tanzania Bara wakiwa tayari wamekosa magoli mengi kupitia kwa washambuliaji wao Amisi Tambwe na Kpah Sherman. Wakati huohuo Michuano ya kimataifa ya tenesi kwa kanda ya Afrika inayofanyika Jijini Dar es salaam Tanzania yamefikia hatua ya fainali ya kwanza. Katika fainali ya mchezaji mmoja mmoja Sada Nahiman wa Burundi alimfunga Mandi Juma Furaji wa Tanzania kwa seti 6-4 7-5.

    Huku Abdoulshakur Kabura wa burundi akipata ushindi kwa seti 4-6 6-4 6-4 dhidi ya Damien Laporte wa Sychelles. Katika michezo mingine Ernest Habiyambere wa Rwanda amemchapa Emanueli Malya wa Tanzania kwa jumla ya seti 4-6 7-6 na 6-4. Yabsira Kadebe wa Ethiopia ameibuka kidedea kwa kumchapa Radjabu Ntambi wa Burundi kwa 6-2 6-2. Kwa upande wa fainali ya wawili wawili Abdoulshakur Kabura na Jonathan Mugisha wa burundi wamewachapa Ryan Randiek na Keen Shan wa Kenya kwa seti 6-1 6-2. Abraham Adelin na Georgina Kemmy wa Tanzania wamepata ushindi wa seti 6-1 6-1 dhidi ya Mwamini Bitungwa na Mariam Mujawiana wa Burundi. Washindi watano wa jumla toka katika kila kundi wataenda kushiriki michuano ya tenesi ya Afrika kwa vijana itayofanyika Nchini Tunisia mwezi Machi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako