Maonyesho ya 12 ya kimataifa ya vifaa vya ulinzi yamemalizika mjini Abu Dhabi, na thamani ya mikataba iliyosainiwa kwenye maonyesho hayo ilifikia dola za kimarekani bilioni 5.
Ujumbe 159 na makampuni 1,200 kutoka nchi 50 duniani wameshiriki kwenye maonyesho hayo ambayo yalitembelewa na watu zaidi ya laki 1, ambapo makampuni 40 ya vifaa vya kijeshi ya China, ikiwa ni pamoja na Kampuni ya Viwanda ya Kaskazini ya China na Kampuni ya Teknolojia ya Baoli.
Wakati huohuo, maonyesho ya 3 ya ulinzi wa baharini na maonyesho ya kwanza ya mifumo isiyoendeshwa na binadamu pia yamemalizika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |