• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Nigeria waibuka mabingwa wa kombe la Afrika la Vijana chini ya miaka 20

    (GMT+08:00) 2015-03-24 14:07:44
    Nigeria wamekuwa mabingwa wa mwaka huu wa taji la Afrika la Vijana wasiozidi umri wa miaka 20. Nigeria ilitawazwa mabingwa baada ya kuigaragaza Senegal bao moja kwa nunge katika fainali za mashindano hayo yaliyofanyika huko Dakar.

    Kiungo wa kati wa ''The Flying Eagles'' Bernard Bulbwa ndiye aliyepachika bao hilo katika kipindi cha kwanza. Kufuatia ushindi huo Nigeria sasa wamewazidi wapinzani wao Misri kwa zaidi ya mataji matatu. Timu hiyo ya Nigeria inaungana na Senegal, Ghana na Mali kuiwakilisha Afrika katika kombe la dunia la vijana wasiozidi umri wa miaka 20. The Flying Eagles wamejumuishwa kwenye kundi E ambapo wanatarajiwa kujiunga na Brazil, Korea Kaskazini na Hungary. Mashindano hayo yataaanza Mei 30 na kukamilika Juni 20 huko New Zealand.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako