• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Barceleona, Bayern waingia waingia nusu fainali ya michuano ya klabu bingwa wa ulaya

    (GMT+08:00) 2015-04-22 15:30:43
    Hatua ya 8 bora ya michuano ya klabu bingwa wa ulaya imeendelea tena jana usiku katika raundi ya pili ya hatua hiyo, ambapo vilabu vya Barceleona waliikaribisha PSG ndani ya Nou Camp na FC Bayern nao walikuwa na mzigo wa kugeuza matokeo ya wiki iliyopita mbele ya FC Porto. FC Barcelona wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani, jana walifanikiwa kuvuka kwenda hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo baada ya kuifunga PSG kwa magoli 2-0, na hivyo kupata ushindi wa jumla wa 5-1. Neymar alifunga magoli yote mawili katika mchezo huo.

    Huko nchini Ujerumani katika uwanja wa Allianz Arena, FC Bayern wamefanikiwa kuiondoa FC Porto kwenye michuano hii kwa ushindi mnoni wa 6-1. Magoli ya Bayern yalifungwa na Alcantara, Boeteng, Lewandoski aliyefunga mawili, Muller na Xabi Alonso akifunga la 6 huku Jackson Martinez akifunga goli moja la Porto – kwa ushindi huo Bayern imeingia nusu fainali ikiwa na jumla ya ushindi wa magoli 8-4. Ligi hii itaendele leo kwa michezo dhidi ya Atletico Madrid vs Real Madrid na mchezo mwingine ni. Juventus vs Monaco.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako