TP Mazembe kutoka (DRC) wako katika Kundi A pamoja na Smouha (Misri), Tetouan (Morocco) na Al Hilal (Sudan).
Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limeamua kupanga ratiba ya michuano hiyo baada ya droo kupigwa kwa ajili ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa, leo mjini Cairo.
Kundi la Algeria ambalo lina asilimia 75 limeondolewa, kwani ES Setif, mabingwa wa Afrika, USM Alger na MC Eulma ziko pamoja na Al Merreikh kutoka (Sudan).
Itakumbukwa kwamba Algeria ni kwa mara ya kwanza katika historia yake, kuwa na wawakilishi watatu katika hatua hii ya mashindano.
Katika Kundi B, TP Mazembe imefanikiwa kuwekwa katika kundi moja na Smouha SC (Misri) pamoja na Moghreb Tetouan kutoka (Morocco) na Al Hilal (Sudan).
Hatua hii ya makundi itachukua muda wa siku sita. Klabu mbili kutoka kila kundi zitachuana katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali, michuano ambayo imepangwa kuchezwa tarehe (25 hadi 27 mwezi Septemba) na mmichuano ya marudiano imepangwa kuchezwa tarehe (02 hadi 4 mwezi Oktoba).
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |