Mashindano hayo yatavutia wanariadha wa mbio fupi na ndefu kutoka ncho mbali mbali barani Afrika.
Tanzania imetoa ithibati ya kushiriki kupitia katibu mkuu wa riadha nchini humo Suleiman Nyambui na miongoni mwa wakimbiaji wa Tanzania wanaotegemewa kushiriki ni pamoja na Fabian Joseph, Mary Naali, Natalia Elisante na Ismail Juma.
Nchi nyingi, ikiwemo Kenya ilio na wanariadha mairi Afrika, zinategemewa kushiriki kwa sababu michuano hiyo itakuwa ni sehemu ya kufuzu kucheza Michezo ya Afrika (All Africa Games) itakayofanyika Congo Brazzaville kuanzania Septemba 4-19 mwaka huu
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |