Juventus wenyeji wa pambano hilo walipata bao lao la kwanza katika dakika ya 8 ya mchezo kupitia kwa Alvaro Morata.
Hata hivyo Cristiano Ronaldo alisawazisha katika dakika ya 27. Matokeo yaliyodumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika.
Juventus walipata goli tena katika dakika ya 57, kutokana na mpira wa adhabu ya penalti, ambapo Carlos Tevez aliifungia timu yake. Hadi kipenga cha mwisho, Juventus 2, Real Madrid mabingwa watetezi 1. Timu hizo zitarudiana tarehe 13 Mei katika uwanja wa Bernabeu, mjini Madrid.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |