Mfalme Abdullah II Bin Hussein wa Jordan jana alikutana na rais Mahmoud Abbas wa Palestina, ambapo walijadili namna ya kuanzishwa tena kwa mchakato wa amani wa Mashariki ya Kati. Mfalme Abdullah II amesisitiza kuwa, Jordan itaendelea kufanya juhudi kwa ajili ya kuanzishwa tena kwa mazungumzo ya amani kati ya Palestina na Israel. Pia amesisitiza kuwa Jordan inapinga kithabiti Israel kuendelea kutekeleza sera ya upande mmoja na vitendo vyake vya uvamizi dhidi ya msikiti wa Aqsa mjini Jerusalem.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |