• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uwekezaji wa moja kwa moja wa China katika nchi za nje waongezeka kwa asilimia 16.3

    (GMT+08:00) 2015-11-16 21:03:19
    Takwimu zilizotolewa na wizara ya Biashara ya China zinaonesha kuwa katika kipindi cha miezi 10 ya mwanzo ya mwaka huu, uwekezaji wa moja kwa moja usio wa kifedha wa China kwa nchi za nje umefikia dola bilioni 95 za kimarekani, ukiongezeka kwa asilimia 16.

    Uwekezaji huo ni wa makampuni zaidi ya elfu 5 ya China yaliyokuwepo katika nchi na sehemu 152 duniani.

    Naibu mkurugenzi wa ofisi ya uwekezaji kwa nje katika wizara ya biashara ya China Bw. Jiang Wenbin amesema miradi ya nje kama vile usafiri, ujenzi wa nyumba, umeme, na mawasiliano ya simu iliyosainiwa iliongezeka kwa kiasi kikubwa, na thamani ya jumla ya miradi hiyo inazidi dola bilioni 108 za kimarekani.

    Takwimu hizo pia zinaonesha kwamba uwekezaji wa China katika sekta ya utengenezaji umeongezeka kwa asilimia 82, na utengenezaji wa simu za mkononi, mashine, kompyuta, vifaa vya mawasiliano zimewekezwa zaidi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako