Bunge la Ulaya limetaka nchi za Umoja wa Ulaya kuwajumuisha watoto wakimbizi kwenye mifumo yao ya kitaifa ya elimu, na kusema kufanya hivyo kutasaidia kupunguza hatari ya vijana kujiunga na makundi yenye msimamo mkali. Pia limetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kutoa kipaumbele kwa elimu inaposhughulikia misukosuko ya wakimbizi kupitia mipango inayolenga kutoa msaada wa kisaikolojia kwa watoto hao na kuwahimiza kujifunza lugha za nchi zinazowapokea ili kuhakikisha kiwango cha juu cha maingiliano.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |