Waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Wang Yi leo hapa Beijing amesema jana usiku makubaliano kuhusu suala la nyuklia la Iran imeanza kutekelezwa rasmi, na jumuiya ya kimataifa imeondoa vikwazo dhidi ya Iran. Amesema kuwa, matokeo hayo hayapatikani kwa urahisi. Kuanzia mwezi Julai mwaka jana nchi sita na Iran zimefanya kazi nyingi za maandalizi kwa ajili ya utekelezaji wa makubaliano hayo, na kuonyesha nia ya kisiasa na ahadi thabiti ya kulinda makubaliano hayo. China inapongeza sana.
Bw. Wang Yi amsema China inapendekeza kuwa pande mbalimbali zinapaswa kutimiza ahadi zilizotoa, kuongeza uaminifu, kuhesimiana na kuelewana katika utekelezaji wa makubaliano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |