Waziri wa mambo ya nje wa China Bw. Wang Yi ambaye anaongozana na rais Xi Jinping wa China katika ziara yake nchini Saudi Arabia leo amekutana na mwenzake wa nchi hiyo Bw. Adel al-Jubeir.
Mawaziri hao wametangaza kuwa, rais Xi Jinping wa China na mfalme Abdulaziz Al Saud wa Saudi Arabia wamekubaliana kuunda kamati ya ngazi ya juu inayoelekeza na kuratibu ushirikiano kati ya pande hizo mbili katika sekta mbalimbali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |