Katibu mkuu wa chama cha mashirika ya ndege cha Afrika Bw Elijah Chingosho amesema mjini Nairobi kuwa nchi zinazomiliki asilimia 85 ya huduma za ndege barani Afrika, zimekubali kufungua soko kwa wenzao barani Afrika. Hatua hiyo inaweza kufanya Afrika iwe na soko moja la safari za ndege kabla ya mwaka 2017.
Hata hivyo Bw Chingosho amesema kuwa changamoto kubwa ya kufungua soko la huduma ya ndege barani Afrika inatoka kwenye nchi zisizo na mashirika ya ndege yenye nguvu, yanayozisukuma serikali za nchi zao kutoruhusu kufungua soko la huduma ya usafiri wa ndege.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |