Msemaji wa polisi ya Burundi Pierre Nkurikiye amesema watu 9 kati ya waliojeruhiwa wako katika hali mahututi, na washambuliaji waliokuwa kwenye pikipiki walirusha guruneti lililokuwa kwenye mfuko wa plastiki na kukimbia. Tukio hilo limetokea karibu na kituo cha polisi mtaani Buyenzi, lakini mashuhuda wamesema inaonekana kituo hicho hakikulengwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |