Mkutano wa mawaziri wa fedha na wakuu wa benki kuu za nchi za G20 uliofungwa jana huko Shanghai, umetoa taarifa ya pamoja, ikisema pande mbalimbali zimekubaliana kuchukua hatua nyingi zaidi katika kukabiliana na changamoto za kiuchumi duniani.
Kwenye mkutano huo, pande mbalimbali zimejadili hali ilivyo ya uchumi wa dunia, muundo wa ongezeko la uchumi, uwekezaji na miundombinu, mfumo wa mambo ya kifedha ya kimataifa, mageuzi ya idara za mambo ya kifedha, ushirikiano wa kimataifa kuhusu ushuru, kukusanya fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya ugaidi na mambo mengineyo, na zimefikia makubaliano mengi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |