Baraza la mawaziri la Kenya limeidhinisha kurefusha reli ya Mombasa-Nairobi hadi Malaba kwenye mpaka wa magharibi mwa nchi hiyo kupitia mji wa Kisumu. Awali reli hiyo inayojengwa na Kampuni ya China ilipangwa kuanzia Mombasa hadi Nairobi, lakini imerefushwa hadi Naivasha. Benki ya Exim ya China ilichangia asilimia 90 ya sehemu ya kwanza ya mradi huo, na fedha zilizobaki zinatolewa na serikali ya Kenya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |