Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bw. Lu Kang alipokutana na waandishi wa habari hii leo amesema:
"Mkutano huu umetoa taarifa ya mwenyekiti kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, hii ni mara ya kwanza katika historia ya kundi la G20. Pande mbalimbali zimeahidi kusaini mapema iwezekanavyo makubaliano ya Paris tarehe 22 Apirili au baada ya siku hiyo, ili kuweka mazingira kwa ajili ya utekelezaji wa makubaliano hayo. Hii inaonesha wajibu na mshikamano wa nchi wanachama wa kundi hilo. Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon amesifu sana kitendo hicho."
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |