• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kundi la G20 lasisitiza tena ahadi zao za kuhimiza ukuaji wa uchumi kwa kutumia sera

    (GMT+08:00) 2016-04-16 18:44:51
    Viongozi wa sekta za fedha kutoka nchi za G20 wamesisitiza tena ahadi zao za kuchochea ukuaji wa uchumi kwa kutumia sera mbalimbali za kifedha na za marekebisho ya muundo.

    Taarifa iliyotolewa Ijumaa na mawaziri wa fedha na wakuu wa benki za nchi za G20 inasema, uchumi wa dunia bado unakabiliwa na shinikizo ya kupungua na hali isiyojulikana.

    Jumanne wiki iliyopita, Shirika la Fedha la Kimataifa IMF limeshusha makadirio yake kuhusu ukuaji wa uchumi kwa mwaka huu hadi asilimia 3.2, likisema uchumi wa dunia unakua kwa kasi ndogo, hali ambayo inafanya uchumi huo ukabiliwe na hatari.

    Taarifa ya G20 aidha inasema migogoro, ugaidi, mawimbi ya wakimbizi na uwezekano wa Uingereza kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya zinaleta utatanishi kwa mazingira ya kiuchumi ya dunia.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako