Mkutano wa kwanza wa Tume ya shughuli za viwanda na biashara ya kundi la G20 umefanyika mjini Washington, Marekani.
Zaidi ya wajumbe 300 waliohudhuria mkutano huo wamejadili ripoti ya mapendekezo itakayowasilishwa katika mkutano wa wakuu wa kundi la G20.
Akihutubia mkutano huo, Naibu mkurugenzi wa Shirika la Fedha la Kimataifa IMF Bw. Zhu Min amesema makampuni binafsi yanatoa mchango mkubwa kwa mambo ya uchumi na fedha duniani, hivyo kuwafanya wanaviwanda kushiriki kwenye majadiliano kuhusu uchumi wa dunia ni muhimu sana.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |