Mkutano mkuu wa kwanza kuhusu ubinadamu duniani umekamilika kwa kutoa ahadi 1,500. Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon amewaambia waandishi wa habari kuwa Umoja huo utaendelea na juhudi za kutimiza malengo ya kazi za ubindamu, kuhimiza nchi wanachama kuonesha ushawishi wao na kuunga mkono juhudi za Umoja wa Mataifa. Umoja wa Mataifa utaitisha mkutano wa ngazi ya juu zaidi kuhusu suala la wakimbizi katika makao makuu ya Umoja huo mjini New York tarehe 19, Septemba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |