Mchezaji bora wa ligi ya mpira wa kikapu nchini Marekani NBA, Stephen Curry, amesema hatokuwamo katika kikosi cha Marekani kwenye michuano ya Olimpiki mjini Rio, Brazil, mwezi Agosti mwaka huu kutokana na majeruha.
Curry alifunga pointi 18, alfajiri ya jana na kuisaidia timu yake ya Golden State Warriors kuongoza kwa ushindi mara wa 2-0 kwenye mchezo wa fainali ya pili, kati ya saba ya ligi ya NBA dhidi ya Cleveland Cavaliers.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |