Kocha mkuu wa klabu ya Yanga, Hans van der Pluijm amesema klabu ya Medeama ya Ghana si timu ya kudharau na wanalazimika kujipanga kwenye mambo mengi sana ili kuhakikisha wanaibuka na ushindi.
Kikosi cha Yanga kitavaana na kikosi cha Medeama katika mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jumamosi Julai 16 mwaka huu.
klabu ya Yanga iko kundi A na inashika mkia huku TP Mazembe ikiwa inaongoza na kufuatiwa na Mo Bejaia na Medeama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |