• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China, Cote d'Ivoire, na India kuandaa kwa pamoja Monyesho ya 13 ya kimataifa ya kampuni ndogo na za ukubwa wa kati

    (GMT+08:00) 2016-07-28 19:32:39
    China kwa kushirikana na Cote d'Ivoire na India, itafanya Monyesho ya 13 ya Kimataifa ya kampuni ndogo na za ukubwa wa kati mwezi Oktoba mwaka huu mjini Guangzhou.

    Naibu katibu wa sekretariati ya Kamati ya maandalizi ya maoneysho hayo Bw. Tian Chuan amesema, idadi ya nchi zinazotaka kushirikiana na China katika kuandaa maonyesho hayo imeongezeka zaidi. Licha ya Cote d'Ivoire, nchi kama Afrika Kusini, Nigeria, Kenya, na Ethiopia zote zimeonesha nia kubwa ya kushiriki kwenye maandalizi ya maonesho hayo, na wajumbe wa nchi hizo watahudhuria maonyesho ya mwaka huu.

    Mkuu wa ofisi ya mambo ya maonyesho hayo Bw. He Zuoxian amesema, maonesho hayo yataweka mabanda 4,600 yenye eneo la jumla mita za mraba laki moja, na kwamba nchi zaidi ya 20 zikiwemo Russia, Japan, Ujerumani na Uturuki, zimethibitisha kushiriki kwenye maonyesho hayo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako