Baada ya kupata tiketi ya kuwania ubingwa wa kandanda Afrika AFCON, Uganda Cranes itafahamu wapinzani wake wa mechi za makundi za Kombe hilo la Afrika Oktoba 19, 2016 jijini Libreville nchini Gabon.
Cranes ya kocha Milutin 'Micho' Sredojevic ilirudi Jumapili katika AFCON kwa mara ya kwanza kabisa tangu imalize makala ya 1978 katika nafasi ya pili baada ya kupiga Comoros 1-0 jijini Kampala.
Kutokana na viwango vyake vya chini vya soka katika Orodha ya washiriki 16 wa makala ya mwaka 2017, Uganda huenda wakajipata katika kundi ngumu linalojumuisha wapinzani kama Ivory Coast na Morocco.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |