• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mwezi ulizaliwa vipi?

    (GMT+08:00) 2016-09-14 09:40:30

    Katika miaka mingi iliyopita wanajimu hawakupata maoni ya pamoja kuhusu jinsi mwezi ulivyozaliwa. Kimsingi waliwahi kutoa nadharia nne kuhusu chanzo cha mwezi.

    Nadharia ya kwanza ni kwamba mwezi uligawanyika kutoka katika dunia yetu. Mwaka 1898, mnajimu George Howard Darwin alisema mwanzoni mwezi ulikuwa ni sehemu moja ya dunia, lakini dunia ilizunguka kwa kasi kupita kiasi na kusababisha mwezi kugawanyika katika dunia. Lakini sampuli za miamba ya mwezi zilizopelekwa duniani na chombo cha anga ya juu zinaonesha kuwa miamba ya mwezi ni tofauti kabisa na ile ya dunia, hivyo nadharia hii si sahihi.

    Nadharia ya pili ni kwamba mwezi ni kimondo kilichovutwa na dunia. Baadhi ya wanajimu wamekanusha nadharia hii, kwani mwezi si mdogo, dunia haina mvuto mkubwa wa kutosha kuvuta kimondo kikubwa kama hiki.

    Nadharia ya tatu inasema hewa na vumbi kwenye mfumo wa jua vilikusanyika pamoja na kuunda mwezi na dunia, hivyo vina chanzo cha pamoja. Lakini nadharia hii pia imekanushwa, kwa sababu sampuli za miamba ya mwezi zinaonesha kwamba mwezi una historia ndefu zaidi kuliko dunia.

    Nadharia ya nne imekubaliwa na watu wengi zaidi, inasema wakati dunia ilipoanza kuundwa, iligongwa na kimondo. Vipande vya kimondo hiki vilikimbilia duniani, lakini kutokana na mvuto wa dunia, havikwenda mbali na kukusanyika pamoja na kuunda mwezi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako