• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China kuimarisha mageuzi ya kifedha baada ya sarafu yake kujiunga na SDR

    (GMT+08:00) 2016-10-01 20:05:36

    Benki kuu ya China imesema kuwa China itaendelea kusukuma mbele mageuzi ya mfumo wa fedha na kufungua mlango zaidi kwa nje, baada ya sarafu yake RMB kuingizwa kwenye utaratibu wa SDR wa Shirika la fedha la kimataifa IMF.

    Ijumaa iliyopita shirika la IMF lilitangaza kundi jipya la sarafu za SDR ikiwemo sarafu ya China Yuan, ambalo limeanza kufanya kazi rasmi leo, likisema kuwa hii ni hatua muhimu ya kihistoria kwa China, shirika la IMF na mfumo wa fedha wa kimataifa.

    Taarifa iliyotolewa na benki kuu ya China kwenye tovuti yake inasema, China inakaribisha hatua hiyo, ambayo itaimarisha uwakilishi, utulivu na mvuto wa utaratibu wa SDR wakati mageuzi ya mfumo wa fedha wa kimataifa yanapoendelezwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako