Huu ni ushindi wa kwanza kwa Hamilton tangu ashiriki mbio za Grand Prix za Ujerumani mwezi Julai na kumfanya awe nyuma ya mshindani wake wa timu moja ya Mercedes kwa pointi 26. Rosberg amemaliza nafasi ya pili baada ya kurejea kwenye nafasi hiyo alipopitwa na dereva wa Red Bull Daniel Ricciardo mwanzoni mwa mbio hizo. Muaustralia huyo amemaliza nafasi ya tatu akifuatiwa na dereva wa Ferrari Sebastian Vettel. Bingwa wa dunia Hamilton sasa ameshinda mbio 50, wakati ambapo Alain Prost alishinda 51 na Michael Schumacher mbio 91ambaye ameshinda mbio nyingi zaidi katika historia yam bio.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |