• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Si binadamu wa kale tu waliotengeneza vipande vya mawe vyenye makali

    (GMT+08:00) 2016-10-25 09:31:21

    Uwezo wa kutengeneza vipande vya mawe vyenye makali na kuvitumia kazini uliwawezesha binadamu wa kale kuishi vizuri duniani. Lakini hivi karibuni wanasayansi waligundua kuwa si binadamu tu wenye uwezo wa kutengeneza vipande hivi.

    Kima aina ya sapajus libidinosus wanaoishi huko Amerika ana uwezo mkubwa wa kutumia mawe. Wanajua kuvunja kokwa kwa mawe, na kuwavutia jike kwa kuwatupia mawe. Dr. Tomos Proffitt wa Chuo Kikuu cha Oxford na wenzake walipotafiti kima hao katika bustani ya taifa ya Serra da Capivara nchini Brazil, waliona kima hao wanaweza kutengeneza vipande vya mawe ambavyo vinafanana na vile vilivyotengenezwa na binadamu wa kale.

    Kima hao wanapenda kugonga jiwe moja kwa jiwe lingine mara kwa mara, na mara nyingi wanafanikiwa kutengeneza vipande vya mawe. Ingawa vipande vya mawe vyenye makali ni vifaa vizuri vya kukatia, lakini kima bado hawajui namna ya kutumia vipande hivi. Watafiti hawajathibitisha lengo la vitendo vya kima hao, lakini wameona kuwa baada ya kugonga mawe, kima hao huyaramba. Dr. Proffitt anafikiri huenda kima hao wanakula unga wa mawe ili kupata lishe ya silicon au wanakula kuvu kwenye mawe.

    Lakini sasa watu wakigundua mabaki ya vipande vya mawe yenye historia ndefu, hawawezi tena kusema moja kwa moja kama vilitengenezwa na binadamu wa kale, wanahitaji kufikiria uwezekano kwamba huenda vilitengenezwa na kima.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako