Mwendesha gari Lewis Hamilton ashinda mashindano ya mbio za magari Formula 1 nchini Mexico.
Hamilton ametumia gari yake aina ya Mercides licha ya gari yake hiyo kupata hitilafu tairi ya mbele, mara tu alipoanza mashindano hayo. mpinzani wake wa karibu Nico Rosberg naye alitumia gari aina ya Mercedes, aliamini kushinda katika mashindano hayo, lakini alijikuta akimaliza kwa kushika nafasi ya 2 nyuma ya Hamilton ambaye ndiye aliyeibuka mshindi na mshindi wa 3 alikuwa Sebastian Vettel aliyetumia gari aina ya Ferrari.
Na sasa tunajiunga naye Thom Wanjala toka Nairobi Kenya, anazungumza na mchambuzi wa soka Abdil Zaka, kuelezea kocha mpya wa AFC Leopard.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |