• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kibarua cha kocha Frank de Boer chaota mbawa klabuni Inter Milan

    (GMT+08:00) 2016-11-03 09:45:25
    Kibarua cha kocha Frank de Boer kimeota mbawa baada ya klabu ya Inter Milan ya Italia kumtimua akiwa ameitumikia klabu hiyo kwa siku 85 pekee ambapo ameshindwa mechi nne ligini.

    Inter kwa sasa wapo nafasi ya 12 Serie A baada ya kushindwa 1-0 Sampdoria juzi Jumapili. Hiyo ilikuwa mechi yao ya nne kushindwa katika mechi tano za ligi walizocheza chini yake msimu huu.

    De Boer mwenye miaka 46, alikuwa beki wa Uholanzi enzi za uchezaji wake na aliwahi kuwa mkufunzi wa Ajax. Alihusishwa na kuhamia klabu za Everton na Southampton majira ya joto.

    Inter leo watakutana na Southampton ligi ndogo ya Ulaya, Europa League. Mkufunzi wa timu ya vijana Stefano Vecchi atakuwa kwenye usukani mechi hiyo. Wakati wa uchezaji wake, alichezea Ajax, Barcelona, Galatasaray na Rangers.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako